Governors Commitment and Plan
Twende Kilifi
Kilifi NGO Portal
Kazi Kilifi
Buy and Rent – Kilifi

Copyright 2024
Kilifi County Government
Karibu Kilifi

Back
Executive > Mashindano ya Quran

Mashindano ya Quran

Company
Elimu ya dini ni msingi muhimu katika malezi na makuzi ya watoto wetu, ikilenga kumjua Mungu, kuimarisha maadili, na kukuza utu mwema.
Nimehudhiria mashindano ya kuhifadhi Kitabu Tukufu cha Allah, Quran, yaliyoleta pamoja washindani 160, yaliyofanyika ukumbi wa Nidhamia, Malindi, chini ya udhamini wa Baraza la Muungano na Ustawi wa Walimu wa Madrasa na Wahubiri wa Kiislamu, Kaunti ndogo ya Malindi. Ahmed AbdulRashid kutoka Markaz Muumin ametangazwa mshindi kwa uwezo wake wa kuhifadhi msahafu wote.
Vipaji hivi vinafaa kuendelezwa kwa ajili ya maendeleo bora ya vijana, jamii, na taifa kwa ujumla. Tunatoa pongezi kwa washindi na wote walioshiriki kufanikisha hafla hii.
Nimeandamana na Gavana Abdulswamad Shariff Nassir ( Mombasa), Idris Dokota ( Katibu Baraza la Mawazri), Hon. Amina Mnyazi – M.P Malindi Hon.Paul Katana ( M.P Kaloleni),Sheikh Juma Ngao(Mwenyekiti KEMNAC) miongoni mwa viongozi wengine .
Avatar
Editor@kilifi.go.ke
Date

March 31, 2024

error: Content is protected !!