Governors Commitment and Plan
Twende Kilifi
Kilifi NGO Portal
Kazi Kilifi
Buy and Rent – Kilifi

Copyright 2024
Kilifi County Government
Karibu Kilifi

Back
Executive > Mazishi ya Suzan Bebora Rabai

Mazishi ya Suzan Bebora Rabai

Company
Kama tunaishi, tunaishi kwa ajili ya Bwana; na pia kama tukifa tunakufa kwa ajili ya Bwana. Kwa hiyo basi, kama tunaishi au kama tunakufa, sisi ni mali ya Bwana. – Warumi 14:8
Niliungana na waombolezaji wakiwemo familia, jamaa na marafiki wa mwenda zake Mama Suzan Kudodola Bebora nyumbani kwao Magombe kwa Bebora, Mazeras, eneo bunge la Rabai.
Mwenda zake atakumbukwa kwa kuwa mcha Mungu, kielelezo chema, mwenye upendo na vile vile mama mkakamavu aliyethamini amani na ustawi wa jamii aliyoishi. Kwa niaba ya Gavana Gideon Maitha Mung’aro na familia yangu, tunatoa rambirambi kwa familia kwa kuondokewa na mpendwa wenu.
Tunawaombea faraja na amani itokayo kwa Mwenyezi Mungu na mzidi kumtumaini yeye kwa kila jambo wakati huu wa msiba na mnapofanya matayarisho ya hafla ya mazishi hapo kesho.
Pumzika katika amani ya Mungu Mama Suzan Kudodola Bebora.
Avatar
Editor@kilifi.go.ke
Date

July 19, 2024

error: Content is protected !!